Latest Updates

WANAUME HUPENDA KUOA MWANAMKE WA AINA HII



 

WANAUME HUPENDA KUOA MWANAMKE WA AINA HII
Habari za wiki hii mpenzi msomaji. Mimi namshukuru Mungu kwa kuweza kunikutanisha na nyinyi kupitia safu hii ambayo pamoja na mambo mengine nazungumzia juu ya mada mbalimbali ambazo zinagusa maisha yetu ya kila siku.
Wiki hii nitazungumazia juu ya aina ya wanawake ambao wanaume wengi hupendelea kuoa. Wanaume wengi wanapofikia hatua ya kuoa si kwamba wanakurupuka tu na kuoa mwanamke yeyote mwenye sura nzuri, bali huchukua muda wao mwingi kuchunguza mambo mengi juu ya wake ambao wanadhani kwamba wanaweza kuwa pamoja kwa kipindi chote cha maisha.
Wanawake wengi wanajisahau na kudhani kwamba kitu kinachoweza kuwafanya wakapata wachumba ni uzuri hivyo kupoteza muda wao kujichubua na kujiremba ili wawavutie wanaume bila kujua kwamba kuolewa ni zaidi ya uzuri.
Hali sasa hivi imebadilika ni tofauti na kipindi cha nyuma ambapo ukiwa na sura nzuri na umbo la kuvutia basi una asilimia 100 za kuolewa. Utafiti ambao nimeufanya unaonesha kwamba zaidi ya uzuri wa tabia na umbo, kuna kuna sifa nyingine za msingi ambazo mwanamke anatakiwa kuwa nazo ili aweze kuwa katika mazingira mazuri ya kupata mchumba wa kumuoa kiasi kwamba asipokuwa nazo ataishia kuchezewa tu lakini haitatokea mtu kumtakiwa kwamba anataka kumuoa.

 
MWEYE MAPENZI YA KWELI
Lengo kubwa la mwanaume kuoa ni kutaka kupata mapenzi ya kweli kutoka kwa mwanamke na ikiwezekana waweze kupata watotoa ambapo watoto mara ndio wamekuwa furaha ya ndoa. Wapo wanawake wengine ambao wanonesha wazi kutokuwa na mapenzi ya kweli bali wanakuwa na mapenzi ya kuzuga. Wanachotaka wao aidha kupata umaarufu tu kwamba yuko na mtu fulani ama kuweza kupata pesa alizonazo mwanaume lakini sio kwamba ana mapenzi ya dhati kutoka moyoni mwake. Mwanamke asiye na mapenzi ya dhati utamgundua tu, muda mwingi utamuona macho yake yako kwenye mfuko wa mwanaume. Akiona kwamba mfuko umetuna utaona anaonesha mapenzi ya hali ya juu lakini pindi hali inapokuwa kubwa mbaya kifedha mapenzi yanaanza kufifia.
Kwanini wanaume wanapenda wana wake wenye mapenzi ya dhati kutoka mioyoni mwao na si kutokana na fedha walizonazo? Hii inatokana na ukweli kwamba maisha  siku zote yanabadilika, kama waswahili wanavyosema, kuna kupanda na kushuka.Sio kwamba kila siku utakuwa na maisha mazuri na kama itatokea hivyo basi ushukuru mungu.Hivyo basi mwanamke wa kuoa lazima afahamu hivyo na awe tayari kuonesha mapenzi yake ya dhati wakati wote wa maisha yao na si kwa kipindi fulani tu cha neema.
 
Si hivyo tu pia asilimia kubwa ya  maisha ya  ndoa yanatawaliwa na mapenzi, kwa hiyo nyanja hiyo inakuwa ya msingi sana kwa wanaume wengi kuiangalia  ili wasije wakajikuta wanaoa mwanamke ambaye baada ya muda mapenzi yanakwenda likizo hali ambayo inaweza kuwafanya wasiishi maisha ya raha mustarehe.
 
WENYE TABIA NZURI
Tabia njema ndio silaha ya maisha, ukiwa na tabia nzuri kila mtu atakupenda, hiyo ni katika maisha ya kawaida. Lakini linapokuja suala na kuoa tabia inakuwa kitu cha awali sana kungaliwa na hiyo inaweza kuwa na ukweli kwa sababu wapo wasichana wazuri wenye mvuto wa aina yake na maumbile mazuri, lakini  wanakosa wanaume wa kuwaoa, ukiuliza kwani utaambiwa  anatabia mbaya. Naweza kusema hilo ndilo limekuwa tatizo kubwa kwa baadhi ya  wanawake kukosa wanaume wa kuwaona. Hakuna mwanaume hata mmoja kati ya wale ambao nimejaribu kuongea naye ambaye ameonesha kulidharau suala hilo la tabia.
Si hivyo tu wapo wanaume  ambao wameingia kichwa kichwa na kuoa kwa kuangalia sura tu bila kujali tabia, matokeo yake baada ya siku chache yanatokea machafuko ya aina yake hali ambayo imepelekea kuvunjika kwa ndoa kutokana na tabia mbaya alizonazo mwanamke.
 
WENYE UCHU NA MAENDELEO
 
Hivi karibuni kumekuwepo na mabadiliko ya aina yake kwa wanaume, wengi sasa hivi hawapendi kabisa kuoa mwanamke ambaye hana kazi yaani 'golikipa'. Kama atakuwa hana kazi basi awe na uchu wa maendeleo kwa kujituma kufanya kazi mbalimbali za kimaendeleo kama vile kilimo kwa wale walio vijijini na biashara ndogondogo kwa wale ambao wako mijijini na hata vijijini. Ile dhana ya kusema mwanamke ni mama wa nyumbani wa kukaa na kujipodoa akimsubiria mwnaume arudi amstarehesha, sasa hivi imepitwa na wakati. Wanaume wengi wanapenda wanawake ambao ni wahangaikaji, wenye ndoto za maendeleo katika maisha yao. Hata kama watakuwa si wafanyakazi lakini wawe wenye kutoa ushauri kwa waume zao juu ya jinsi gani wafanye ili wafanikiwe.
 
WASIOPENDA MAKUU
 
Kuna  wanawake wengine wanakuwa na tabia za ajabu sana kiasi kwamba yaweza kuwa kero kwa wanaume. Wapo wanawake ambao wanapenda makuu bila kujali hali halisi ilivyo. Kuna wanawake naweza kusema wana tamaa, kila wikiendi utamsikia "leo tunakwenda wapi dear?"  Akimuona rafiki yake kanunua simu ya laki tatu na yeye utamsikia akisema, ‘na mimi naomba uninunulie simu kama  ya Grace’. Ukienda naye Pub anakuambia, "mimi sinywi pombe za chupa natumia za kopo tena Heineken’. Yeye hajali kiasi cha pesa mwanaume alicho  nacho na usipotekelezea anachukia na anaweza hata kupunguza mapenzi.

 
Wanawake kama hawa wako katika mazingira magumu sana ya kuweza kupata wanaume wa  kuwaoa.  Mara nyingi katika maisha fedha huzungumza, kama mwanaume atakuwa na pesa ya kutosha itakuwa rahisi sana kwa mwanamke kupata kila atakachopenda lakini si kwa kumwambia mimi nataka kitu fulani.Mwanaune mwenyewe utamsikia akisema, ‘unataka nikununulie simu ya aina gani, au leo unataka twende wapi?’ hapo ndipo utakuwa na nafasi ya kusema, ‘mimi nataka uninunulie simu kama ya fulani ama leo nataka twende sehemu fulani.’
Wanaume ni warahisi sana wa kuwapatia wale ambao wanatarajia kuwaoa chochote ambacho watahitaji kama tu pesa haitakuwa  tatizo. Kitu ambacho kinawaudhi wanaume wengi  ni ile tabia ya mwanamke kupenda mambo makubwa bila kuangalia uwezo uliopo kwa mwanume.
Kuna wanawake wengine wao si wasemaji kabisa, yeye anasubiri leo amemletea hiki, anapokea na kushukuru, kesho akiambiwa twende beach anakubali. Au wengine wanasubiri mpaka waulizwe wanataka nini, ndio wanasema.
Sisemi kwamba uwe mkimya tu hata kama una shida ya kitu fulani na unafahamu kwamba ukimweleza mwenza wako anaweza kukusaidia, hapana! kama unaona kwamba uwezekano wa kupata kile ambacho unakihitaji upo mweleze kwa utaratibu naamini atakuelewa na kukutimizia.Tabia ambayo hawaipendi wanaume wengi ni ile ya kulazimisha ufanyiwe kitu fulani wakati inawezekana uwezekano haupo.
 
WAVUMILIVU
Wapo wanawake ambao sio wavumilivu kabisa katika maisha.Tunajua kwamba maisha siku zote hayatabiriki, yanaweza kutokea matatizo ya kiafya ama kifedha.Huu ndio wakati wa kuona uvumilivu wa mtu.Kama mwanamke anatarajia kwamba siku zote ni za raha tu na pindi matatizo yanapotokea anachukua uamuzi wa kumtoroka mwanume, huyo siyo mwanamke wa kuoa.Wangapi leo hii huwatoroka waume zao pindi inapotea kuumwa, kufilisika ama kupatwa na tatizo lolote ambalo kwa namna moja ama nyingine yanaweza kuwafanya maisha yao kutingishika?
 
Uvumilivu kwa mwanamke utakuwepo kama tu atakuwa na mapenzi ya dhati kama nilivyozungumza hapo awali. Mwanamke mweye mapenzi ya dhati ni lazima atakuwa mvumilivu na atakuwa tayari kuishi katika maisha ya aina yoyote, yawe ya raha ama ya starehe.Hawa ndio wale ambao wanaume wengi wengependa kuwa nao maishani mwao.
 
Licha ya kupenda kuoa wanawake amabo wana tabia hizo nilizozitaja hapo juu, wanachukizwa sana na wanawake ambao wanavijitabia vidogo vidogo ambavyo kimsingi havikubaliki katka jamii.Tabia hizo ni kama wambea, wasio wakweli na wawazi, wasioridhika, wagumu kusamehe na wapesi wa kuchukia, wagomvi na wenye roho ya kwanini.
 Utafiti huu umefanyikwa kwa baadhi ya wanaume ambao wanatarajia kuoa wanawake ambao wanaoishi katika maeneo mbalimbali jijini Dar-es-Salaam. Kwa maana hiyo basi hiyo iwe changamoto kwa wanawake. Wajue kwamba wanaume wanafurahi kuwa na wanawake wa aina gani. Hata kama utakuwa umeshaolewa, kama kuna wakati kunakuwa na kutokuelewana baina yenu, chunguza yawezekana kwamba unakosa mojawapo ya tabia ambazo nimezitaja hapo juu. Waweza kubadilika kwani inawezekana.

Fedha, uzuri si kinga ya mapenzi, kuna kitu cha ziada

Fedha, uzuri si kinga ya mapenzi, kuna kitu cha ziada



WAKATI akili yangu ikianza kupata ufahamu, nilikuwa natatizika na kuwaza kitu gani hasa katika mapenzi kinaweza kumfanya mtu atulie ndani ya penzi lake. Niliamini kuwa na fedha ndiyo dawa ya mtu kumtuliza mpenzi wake au kwa mwanamke kuwa mzuri na mwenye sifa zote, ndiyo dawa ya kumfanya mpenzi wako atulie.
Baada ya kukua na kuingia katika dunia ya ufahamu wenye mitihani mingi ya mapenzi, nimegundua kuna utofauti mkubwa katika vitu nilivyoviwaza.

Wakati nakua, nilikutana na matukio ambayo niliona kama ngamia kupita kwenye tundu la sindano, lakini baada ya kupevuka, nilipata majibu ya maswali yaliyonisumbua kipindi kile cha utoto.
Sikuamini mke wa tajiri kufanya mapenzi na muuza mchicha, mwanaume mwenye mke mzuri kutembea na changudoa au msichana wa kazi asiyejua kuvaa wala kuoga.
Baada ya kuingia katika kazi hii ya kukumbushana mambo ya mapenzi, nilipata maswali mawili ya watu wawili tofauti lakini yalikuwa na jibu moja.

Mmoja alilalamika ana mke, anamhudumia kila kitu ikiwemo familia yake lakini alichomlipa ni kutembea na mtu asiye na mbele wala nyuma. Mwingine alilalamika kuhusu mpenzi wake kutembea na mwanamke wa nyumba ya pili ambaye haufikii hata mguu wake kwa uzuri.
Kabla ya kulizungumzia hilo, nirudi kwao kuwaeleza kukosa uamini hakuangalii katembea na tajiri au mwanamke anayekushinda uzuri, kutoka nje ya uhusiano au ndoa ni kosa kwa vile penzi ni la watu walioridhiana au kuoana wakiwemo waliooa wake zaidi ya mmoja.

Leo nawajibu wote kuwa fedha au uzuri wa mtu havibebi ndoa au uhusiano. Nimekuwa muumini mzuri wa kuwaeleza penzi la kweli lipo vipi, mapenzi ni upendo wa dhati kutoka moyoni, kuwa tayari kujilinda na kujiheshimu bila kujali una fedha au ni mwanamke mzuri.
Mapenzi ni mbegu inayohitaji udongo wenye rutuba ya upendo ili mbegu hiyo imee. Siku zote mwenye mapenzi ya kweli humuangalia mtu, si kitu.

Tajiri na fedha zake asipopendwa huwa katika mateso na kukonda wakati ana kila kitu. Penzi la kweli halinunuliwi kwa gharama yoyote.
Tabia ya asili huwa sawa na moto unaowaka kwenye pamba, ukitoa moshi ujue hakuna kilicho salama. Wapo watu wasiokuwa na mapenzi ya dhati, utakuta mtu anajifanya anakupenda ukiwa naye lakini mkiachana hana habari na wewe, hata kama mnakaa nyumba moja na kulala kitanda kimoja.
Mtu anapoamua kutoka nje ya ndoa wakati ndani ana mke mzuri au mume wa ukweli anayempa kila kitu, kuna mawili:
Mosi:
Huenda mwanamke aliyenaye alimtamani kutokana na sura na umbile lake na hakumpenda kwa dhati. Matokeo yake baada ya kumchoka, mwanamke huonekana hafai na hukaa naye kimazoea.
Upande wa mwanamke, naye huenda amekwenda kwa mwanaume kutokana na kujua ana fedha lakini anakuwa hana mapenzi naye. Hapo lazima atatafuta penzi la nje ili afurahishe nafsi yake, kwa hiyo watu hawa kutoka nje sishangai.
Pili:
Tabia ya kutoridhika na mpenzi mmoja, watu wa aina hii huwa hawajisikii kula kitu cha aina moja kwa muda mrefu, lazima atatafuta mtu wa kumfanya abadili mboga.
Vitu hivi vyote huwa vinawachanganya watu, hasa wale wanaoamini kuwa mwanaume anapokuwa na fedha au mwanamke anapokuwa mzuri, ni kila kitu katika mapenzi.
Mapenzi ni bahati, hasa kumpata uliyemkusudia, basi muombe Mungu utakayemchagua naye awe kweli amekukubali, hata ukiwa mbali kila mmoja amlindie mwenzake heshima, kwa kutanguliza uaminifu mbele.

Sinta, Dida na Mange ndani ya Bifu zito.


  I THINK WENGI WETU TULIAMUA KUMU IGNORE TU HUYU MBWA KOKO......KAMA MIMI NDO KABISAAAAA YANI NILIKUWA NISHASEMA NGOJA NIFANYE KAMA HAYUPO HAI...... JAMANI
KILA SIKU LAZIMA ANITUKANE KWENYE COMMENTS ZAKE? NILIM CONTACT KISTAARABU NIKAMWAMBIA SINTA ACHANA NA MIMI, SIKUJUI TUHESHIMIANE, ILA WAPI JITU HALIELEWI.
SIJUI BLOG YAKE HAINOGI BILA KUMTAJA MANGE KIMAMBI. ALAFU UKILIAMBIA ETI LINASEMA SIO MIMI NAWEKA COMMENTS NI ADMINISTRATOR. SURA KAMA ADMINISTRATOR UNA HELA YA KUWEKA ADMINISTRATOR WEWE. MFYUUUUU.....

MIJITU MINGINE BWANA, YANI LAST WEEK NILIBOREKA KIDOGO NKAMZABUE VIBAO. JITU LINAJUA KABISA STORY NI ZA UONGO SASA ANAWEKA COMMENTS ILI IWAJE? BORA HATA BASI ANIFATE FATE MIMI, SOMETIMES ANAWEKA HATA COMMENTS ZA KUTUKANA
WATU AMBAO HATA HAWAJUI JUST BECAUSE HAO WATU WANA ISSUE NA MIE. YANI LAST WEEK NILISEMA NGOJA NKAMZABUE MABAO TUTAHESHIMIANA NIKAPELEKWA HADI KWAKE KANAKAA SINZA PALE BAMAGA, YANI HAPO ANAPOKAA TU NILIMUONEA HURUMA. NKAONYESHA NA HICHO KIBIRITI CHAKE ANACHOENDESHA, YANI NIKASEMA MASKINI YA MUNGU ADHABU TAYARI ANAYO SINA HAJA HATA YA KUMUONGELESHA....KHA!!!
WATU MNAAMBIWA MASHAUZI YANATAKA PESA HAMSIKIIII, MTU UNAJISHAUA WAKATI HUNA MBELE WALA NYUMA, UUNACHEKESHA WALIONUNA TU.UNAJISHAUA NA VINGUO VYA MTUMBA??? MFYUUUUUU, SHENZI KABISA....YANI NAONA HATA AIBU NIMEKAA HAPA NAANDIKA ARTICLE YA YULE MJINGA. ILA LAKINI MTU HAONI KWAMA ANAKUWA IGNORED, KILA SIKU ANANITUKANA ON HER BLOG BUT I IGNORE HER, HATA SIKU MOJA HUWEZI KUKUTA COMMENTS ZA YULE SINTA. HAJIULIZI KWANINI? ANAJIFANYA ANAJUA KUONGELEA MAMBO YA WATU YAKE TUKIONGELEA HAPA TUTAYAMALIZA?
SINTA KUBALI MAISHA YAKO, WEWE NI MTANZANIA WA KIMA CHA CHINI THATS UR STATUS NA SIO MBAYA ,JUST JIKUBALI UNACHEKESHA SANA UNAPOANZA KUTAKA KUWA MATAWI WAKATI YOU DONT HAVE ANYTHING.
HUYU NYAU ALIKUTANA NA MDOGO WA RAFIKI YANGU KWENYE NDEGE ON HER WAY TO UGANDA. KATIKA MAONGEZI HUYO MTOTO AKAMWMABIA AMEFIKIA SERENA HOTEL NA BABAKE. BASI SINTA ASIENDE HADI SERENA HOTEL KUMFATA HUYO MDOGO WA RAFIKI YANGU, ETI NAOMBA KWENDA CHUMBANI KWAKO NIKAPIGE PICHA NIWEKE KWENYE BLOG. HIVI HUYU MTU ANA AKILI KWELI??? JAMANI KAMA HUKUBARIKIWA KUWA NA MAISHA YA JUU EMBU YAKUBALI YAKO TU.
WEWE SINTA KUTAKA KUSHINDA NA MANGE KIMAMBI NI SAWA NA KONDOO ATAKE KUSHINDANA NA SIMBA...CHIEF UTAKUWA UNATANIA....
YOU WILL NEVER BE ME, HATA KARIBU YANGU HUTOFIKA UTAKACHOWEZA KUFANYA NI KUNITUKANA KWENYE COMMENTS ALAFU UJIDAI ETI NI WATU WANANITUKANA....
MBWA MKUBWA MTU SINA BEEF NA WEWE, SIJAWHAI KUGOMBANA NA WEWE, UNANIFATAFATA NINI ?????? NISHAKWAMBIA KISTAARABU MARA MIA KIDOGO HUSIKIIII... ILA UNACHOKITAFUTA KWANGU UTAKIPATA... TENA SHUKURU SIKAI DAR ,
MAANA NIKIJA DAR NIPO BUSY KUTAFUTE MAHELA STAKI KUPOTEZA MUDA POLISI LA SIVYO NGEKUWA NISHAKUTENGUA KIUNO NYAU WE.

HIVI NA NYIE KINA DIDA NA WENGINE MNAOSUMBULIWA NA HUYU PANYA HIVI MNASHINDWA KUMFUNZA ADABU MTU MNAISHI NAE HAPA HAPA TOWN. SIKU MOJA MKAMATENI MUMPE KIBANOO MUMTOE NA NGUO MUMPIGE PICHA MNITUMIE NIWEKE HUMU....
ALAFU MUMFANYIE NA KITU MBAYA MAANA HUYU NAHISI ANASUMBULIWA NA NYEGE TU....HIKI KIHEREHERE ALICHONACHO NI NYEGE ZINAMSUMBUA...ANACHOKITAFUTA ATAKIPATA VERY SOON...." 

MAKUNDI YA WANAWAKE NA MITAZAMO YAO KWA WANAUME

MAKUNDI YA WANAWAKE NA MITAZAMO YAO KWA WANAUME


Ogopa sana mwanamke akikuona wewe ni tatizo, hilo huwa linajengeka na kuishi kwa muda mrefu ndani ya kichwa chake.
Mara chache wanawake ambao huitwa akina mama wa nyumbani, kwa maana ofisi zao ni majukumu ya ndani ya familia peke yake, hujitutumua katika eneo la faragha lakini nao siyo wote. Inapotokea akazaa, ndiyo hushindwa kabisa kuonesha hata yale makeke kiduchu ambayo awali aliyaonesha.




Ukiweka pembeni suala la faragha, wanawake wa kundi hili huwa wanapenda sana. Kwa kawaida,
wakishakita nyoyo zao, huwa hawatazami kwingine. Ni wazuri mno katika kipengele cha kuhimili vishawishi. Wanaweza kusumbuliwa kwa kutongozwa lakini wakabaki imara bila hata kuwashirikisha waume zao.

BAHATI MBAYA 
Wao ni waaminifu lakini kutokana na misimamo yao na kutoyapa kipaumbele mapenzi ya kitandani, hujikuta wakisalitiwa mara nyingi sana. Maajabu yaliyopo ndani yao ni kuwa inawezekana kabisa akajua kwamba mume wake ni msaliti lakini asichukue hatua yoyote, zaidi ya kupigania ustawi wa familia yake.
Wanaweza kukosa tendo la unyumba kwa muda mrefu kutokana na waume zao kuwa ‘bize’ na nyumba ndogo, wakirudi nyumbani wanakuwa wamechoka hata hakuna habari ya kuulizana haki ya ndoa. Maajabu mengine kwa wanawake wa kundi hili ni kuwa wanaweza kunyamaza, wakakaa muda mrefu bila kushiriki tendo bila kuzalisha migogoro ndani ya nyumba.
Wao ni wazalishaji mali, tatizo linalowatesa wanawake wengi wa kundi hili ni kwamba uzalishaji wao, huvunwa na wengine kutokana na tamaa, kiburi na ubabe wa wanaume wao. Hili nalo huvumilia na mara nyingi hujitahidi kupambana na presha ya ubadhirifu wa waume zao kwa ajili ya kuhakikisha maisha ya watoto hayaharibiki.
Janga kubwa zaidi ni kwamba wanawake wa kundi hili huachwa na kusababisha kile ambacho walikichuma, wakakidhibiti kisipotee kwa ajili ya maisha ya kesho, kitumiwe na wengine kiulaini. Sababu kubwa ya wanawake hawa kuachwa pamoja na ukweli kwamba wao ndiyo ‘wife materials’ ni hii;
waume zao husaliti ndoa na kwenda kujirusha na wanawake wa nje (nyumba ndogo), huko hunogewa kiasi kwamba mapenzi yote ya familia zao, huyahamishia nyumba ndogo. Kama hiyo haitoshi, mwanaume huanza makeke mpaka ndoa inapovunjika.
Pindi ndoa inapovunjika, mwanaume humtimua mwanamke kwenye nyumba kisha kujimilisha kila kitu ambacho walichuma pamoja. Mwisho kabisa, mke hubaki hana chochote, akimuacha mwanamke mwenzake akifaidi matunda ya jasho, maarifa na ubunifu wake.
Kitu kikubwa ambacho wanaume huwa hawajui ni kwamba safari moja huanzisha nyingine. Kwamba wanapoanza uhusiano wa nje, hudhani kuwa yatakuwa mapenzi ya juujuu lakini huko nako, hao wanawake huanza kukaba mpaka kivuli, wakitaka haki kuliko wake wa ndoa.
Ni kipindi ambacho wanaume hukosa misimamo na kutetereka. Mke wa nyumbani anamtaka na nyumba ndogo anaihitaji. Mke wa nyumbani huwa hajui kuhusu haya mapambano, kwa hiyo huendelea kuishi maisha yaleyale ya kawaida bila kujua kuwa yanamwathiri.
Nyumba ndogo, yenyewe huongeza makeke kwa sababu inakuwa inajua kuhusu mapambano yaliyopo. Mwisho kabisa, mwanaume huona kwamba mke wa nyumbani hana burudani, kwa hiyo hufanya uamuzi wa kijinga zaidi kwa kuvunja nyumba na kumtimua mke wa ndoa.
Wanaume wengi waliofanya matukio ya aina hii, baada ya miezi michache walijuta, baada ya kubaini kwamba yule aliyemfanya akavunja nyumba yake, hakuwa mwanamke bali gubegube. Pamoja na hayo, ukweli ni kwamba mara nyingi wanawake wa kundi hili hawathaminiki.
Wanawake wa kundi hili ni almasi lakini kwa macho ya kawaida, unaweza kudhani ni chupa.

SABABU 7 KWANINI HUTAKIWI KUFANYA MAPENZI KABLA YA NDOA JAPO NAJUA UNA MIHAMU GUNIA ZIMA NA UNAHISI HUWEZI KUACHA UTAMU HUO

SABABU 7 KWANINI HUTAKIWI KUFANYA MAPENZI KABLA YA NDOA JAPO NAJUA UNA MIHAMU GUNIA ZIMA NA UNAHISI HUWEZI KUACHA UTAMU HUO


Najua hii topic ni msala mtupu! Hilo nalitambua lakini inabidi tu hata hili lisemwe,usiponielewa leo utanielewa tu siku za usoni lakini usiseme sikukwambia


Mimi na wewe wote ni wahanga wa Pre-mature Sex...Kwa wale mliooa(nna uhakika wengi wenu kama sio wote) Mligonga kitu kabla ya muda,au sio?


Sasa mzigo ndo huu hapa...Kuna sababu 7 kwanini tunashauriwa tusifanye Mapenzi kabla ya ndoa....Vitabu vya Dini vimeandika hili na Kukataza lakini amri inavunjwa kama kawa utadhani Kitabu cha Kutoka 20:14 kimefutika kwenye Biblia....Kile kilichokatazwa ndo kinapendwaaaaa,kitamuuuuu,na watu hawataki kukubali kwamba inabidi kiachwe!


Ubishi huu kuhusu kula tunda ndio uliotucost Binadamu kufika hapa tulipo leo...Kosa lileeee la Adamu kupewa Tunda na Eva,baada ya Ibilisi kumdanganya Eva kwamba Tunda lina Mzuka ile mbaya na hata Mungu anajua ndo maana kawabania...uongo ulikuwa mtamu Eva akajaa kimiani..Matokeo yake ndo haya...Adam kafukuzwa Edeni,tumerithi Dhambi na kero chungu nzima...kifo hakikuwa kwenye Plan ya Mungu ila ni adhabu ya uleee uongo wa mwanzo,lakini HATUKOMI wazeee tuko bize kufanya REMIX ya mambo yaleyale aliyofanya ADAM na EVA kule EDENI halafu tunatetea eti haiwezekani,Mungu anajua alichoumba usimfundishe kazi!


SABABU YA 1:IMEKATAZWA NA MUNGU


Sababu ya Kwanza kwanini hatutakiwi kufanya Mapenzi kabla ya ndoa ni kwa sababu MUNGU HAPENDI....Amekataa...Na amekataa sio kwamba hajui Sex ni Tamu,....Anajua utamu woteee unaousikia ukifanya mapenzi...anajua raha unayopata ukiwa unacheza kile kiduku pale bed kwa mbwembwe...Anajua zile hisia unazofeel na nini kinatokea ukifanya,ANAJUA...yeye ndo ameziumba zile hisia,USIMFUNDISHE MUNGU KAZI YA KUUMBA! Alikuumba akijua una Hormone ambazo zitakusumbua lakini vilevile amekupa uwezo wa kuzishinda...Mungu hawezi kuweka jaribu ambalo halina Mlango,kama alisema usifanye basi anajua uwezo wa kutofanya upo!
Tutabisha weeee,ooh haiwezekani,kuna watu hawafanyi na wapo,wanapumua kama wewe,wanamtii Mungu na wanaishi..hawafi,na wanakuja wanaoa na mambo wanakula kama kawa...Zile stori usipofanya sijui ufutio unapotea,mara hivi,ni Plan za shetani tu kama alivyomdanganya Eva akajaa kimiani,anakujaza na wewe uamini ili upotee.USIKUBALI


SABABU YA 2:UTAMU WA HONEYMOON KWISHNEY


Utakapooa, utaenda Honeymoon...Nia ya honeymoon ni wewe kupewa fursa ya kutoa gundi kwa mara ya kwanza...Kumbe gundi umeacha Machimachi Guest House miaka mia8 nyuma


UNAENDA HONEYMOON KUFANYA NINI??KUMDANGANYA NANI??


Hizo hela za Kamati ya Maandalizi watu wanakuandalia kwenda Honeymoon wakati Ramani nzima ya huyo mkeo na mmeo USED unaijua hata ukifumba macho.KATAA HIYO!


SABABU YA 3: UTAKUWA NA AFYA KIROHO


Tunaishi kwa ajili ya Mungu...tuko hai kwa sababu Mungu ametuacha na kutupa nafasi ya kurekebisha maisha...Ukifa leo utakwenda wapi?Umewahi kujiuliza??
Hauko hai kwa sababu wewe ni mwema sana mbele za Mungu...As long as uko hai inabidi uishi vile ambavyo Mungu anataka uishi...MAISHA SAFI MBELE ZAKE!
Na ni ukweli usiopingika kwamba dhambi hii ya NGONO/UTAMU/UZINZI ndio namba 1 katika kuharibu maisha ya kiroho ya Watu...Hii dhambi ndo Weapon namba 1 ambayo Ibilisi anaitumia kumaliza watu.Laiti hii isingekuwa dhambi basi watu wengi sana wangeingia Mbinguni,Wengi sana...Lakini hali ni mbaya sana...
Naweza kuthubutu kusema Afya yako ya Kiroho inategemeana na ushiriki wako kwenye Ngono au La.ukishinda hii,siamini kuna dhambi itakuwa ngumu kwako kushinda,Jaribu uone!
Unaikosa Mbingu hivihivi kisa pale katikati....WAZA UPYA!Tangu uanze kuifanya hiyo kiu imeisha???Mbona unafanya na unafanya na kufanya haiishi,uskiacha utakufa??Its not late to start over,na uzuri wa Mungu ukitubu,anafuta zoteeee za nyuma unakuwa mpya.You can start afresh LEO!


SABABU YA 4:NI NZURI KWA AFYA YA KIMWILI


Hapa napo imekuwa mgogoro.mwanzoni watu walisema aaaah ntakaaje na Sweetie wangu bila kufanya,wakahalalisha...wamefanya weeeee wamechokana...wakaanza kuiba nje,na wapenzi wengine,na kwa sababu umekuwa sugu huoni tabu kuongeza listi...Ishu inakuja Je, hiyo listi yako iko salama???


Watu wengi wamepata pancha hapo katikati,wamefikia muda wanataka kutulia na kufunga ndoa kuanzisha familia...LOH!AFYA MGOGORO!Siku hizi magonjwa ni mengi sana,acha tu Ngoma inayozingua kila kona,kuna magonjwa ya Zinaa ambayo unaweza ukaletewa na bila kuyatibu vizuri ukaharibu vizazi ile mbaya.....Kuna ishu za mimba,maana mechi siku hizi pekupeku tu...ETI MNAAMINIANA,peku pekua mara kitu kimejaa...wote ndo mnagundua hamko tayari kwa mtoto!Upuuzi mwingine huo...Mko tayari kukata kiuno ila result za kiuno hutaki...Utafanyaje mtihani halafu useme hutaki majibu??utajuaje umefaulu au kufeli??Mapenzi bwana!Mwanamke wa watu analazimika kutoa mimba maskini,mwisho wa siku mkibahatika kuoana hampati mtoto,HALFU UTASEMA WHY ME LORD???KWELI???Au mtoto wa kike anaolewa na mtu mwingine,tayari ushamsababishia kimeo kwenye ndoa yake,na haya yako kila kona wala sio mapya.WAZA UPYA!


SABABU YA 5:LINDA HISIA ZAKO


Unampenda mtu unafanya nae Mapenzi...mnaachana,unapanga misururu watu wengi kama msururu wa wateja wa NMB kwenye ATM...Wote hawa unatumia moyo huohuo,hisia hiyohiyo,wote umewaonja,wamekupa different tastes,kama mia7 hivi....wote wamekutenda,Hisia zako zinakuwa na rangi kibaooooo,hata hukumbuki moja kati ya hizo ipi sahihi....
Nakutana na watu wanasema hawawezi kupenda tena,kia wametendwa....Sio hivyo...Sehemu ya hisia ishatiwa shoti,kila mtu kaja na bisibisi yake anachomeka tu,size 17 twendeeee size 44 twendeeee,haueleweki hisia zako zimefikia size ngapi,maana kuna waliozi-under size,na wengine wameku-oversize...Umeshakuwa emotionally unhealthy....


Kwanini usitulie uje utumie hisia zako kiusahihi na mtu sahihi???kwanza hawa unaosex nao wengi hata wazo la kuao hamna,wanakutumia tu bureee bureeee,ukimwambia tu twende home nikutambulishe anajitetea  na maneno lukuki kama konda wa Mazese-Mburahati,ndo utajua utatumiwa tu kama condom,kisha kitanda chako jalalani!


SABABU YA 6: UVUMILIVU NI TESTI NZURI YA UPENDO WA KWELI


Hapa hata sina haja ya maelezo mengi...Mtu mvumilivu huonyesha nia ya dhati na upendo wa kweli..Ila mtu anayekurupuka tu huyooo ndani ya Shuka,utajua tu penzi lake ni la ki-shuka shuka zaidi.


SABABU YA 7: BARAKA ZA MUNGU MLIYEMTII NA UTULIVU WA NDOA


Ukimtii Mungu huwa anatoa baraka zake...Na kinyume chake ni dhahiri...


Wle wanaomuamini Mungu na kufanikiwa kufikia hapa,maisha yao yanakuwaga tofauti kabisa na wale walioishi maisha ya kibiriti-Ngoma Style.


Watu mmetoka tangu urafiki mnaibatua amri ya 6 bila huruma....Sasa mnafika kwenye ndoa mmechokana,Ladha yote imakwisha,,Mke hana jipya la kukupa...Hakuna machejo ya Mme usiyoyajua....NO EXCITEMENT.


Sishangai kuona Mwanaume ameoa anacheat...Hamna jipya,Mke anabakia tu kuwa Kiwanda cha kufyatua Watoto lakini INTIMACY YA NDOA HAKUNA. Anaamua kujaribu ladha zingine!


Na effect za Mwanaume asiye na Intimacy na mkewe zitaonekana hata kwa Mkewe in due time...Hatampa haki yake kadri inavyopaswa,na mwishowe mkewe atachoka kulishwa Makombo,anayoyajua kwa Nusu Karne huko nyuma...


Kifuatacho hapo ni wote kugeuka CHEATERS...Mke anapiga show za nje kwa wizi...Mme nae anakamua mechi za Mchangani nje kwa kujiiba...Wote hawa wanajaribu kupasha misuli nje maana ndani Gym imeishiwa vifaa...Wanajifanya wanapasha moto Kiporo kilichochacha...Kamwe hiyo ndoa itakuwa ngumu sana kusimama tests of Time!




ARGUMENTS
Wengi wata-argue kwamba Maadili yanachangia.NAKUBALI,Siku hizi ni ngumu sana kumuamini Mpenzi kwamba atavumilia,ndio maana Wanawake wameamua kujitoa Sadaka kutoa tunda kama njia ya kuwin penzi la wanaume...UONGO!Penzi la Mwanaume halishikwi kwa kumpa Tunda...Kama anakupenda WEWE atakaa,kama alipenda TUNDA atakwenda...Simple Rule....Mwanaume anapaswa akupende WEWE kwanza na Sio ulichonacho Wewe...Afterall kama ana ana nia na hicho kitu,si atakimilikisha kuwa chake Milele na milele??sasa anakiwahi cha nini??kuku wa Kwako ya nini Manati??


Na wanaume pia,wanalalamika wanawake hawaaminiki,wana roho ndogo...Wewe unamtunza hupigi show unadhani kwamba anakutunzia unashangaa anakuja bwege flani anakula mali yako kiulaini,Roho inauma,so bora upige show ili hata ukiporwa,ah fresh mlinganyo umekaa poa.


Maadili yanachangia lakini na Ibilisi kwa kulitambua hilo,ameinvest hapohapo kwenye LOST FAITH ya Maadili,na anawachapa watu bila huruma.


Mimi nimemaliza hapa..Ukiamua kunisikiliza na kuamini Mungu na akubariki,ila nikiwa kama Jogoo anawahi kuamka lakini hafungui mlango haya..

Mapenzi ni fursa, iheshimu kwa maana haiji mara mbili

Mapenzi ni fursa, iheshimu kwa maana haiji mara mbili



Na Luqman Maloto
Nikuombe msomaji wangu kwamba unaposoma makala haya, soma kwa mtindo wa katikati ya mstari (between the line). Kuna somo kubwa mno kwenye mada hii kwa sababu wengi wapo kwenye mateso makubwa ya kimapenzi kutokana na makosa yao wenyewe.
Ukisoma ujasiriamali, utaelekezwa kwamba mafanikio yako yatatokana pia na namna ulivyo na nidhamu katika fursa unazopata. Inawezekana ukawa na bahati kwenye maisha lakini utabaki kuwa si lolote endapo hutatumia nafasi zako vizuri.

Kama maisha, ndivyo yalivyo mapenzi. Hayatanyooka, wala hayatakaa vema upande wako ikiwa hutakuwa na heshima kwa fursa utakazopata. Si suala la ujana au kujipanga, muhimu kwako ni kuheshimu kile kilichopo jirani yako. Zingatia: Mapenzi ni changamoto nzito.
Ukichezea penzi lako leo kwa sababu unazozijua wewe, tambua kwamba halitakaa kwako daima. Kama yalivyo maisha kwamba yapo mfano wa kioo, ukiyachekea yanacheka, ukiyanunia nayo yananuna. Ndivyo na mapenzi yalivyo. Ukiyachezea, nayo yatakuchezea kweli.
Unapaswa kuyaheshimu. Heshima ya mapenzi ni kumtunuku mapenzi ya kweli huyo ambaye amekujia na mapenzi yake. Umethibitisha anakupenda kweli, sasa kinachokuwasha nini mpaka uunyanyase moyo wake? Fumba macho, mara nyingi bahati huwa haiji mara mbili.
Inawezekana mwenzi wako wa leo ndiye mwenye mapenzi ya kweli. Ila wewe unausimanga moyo wake kwa sababu hana fedha. Unakwenda kuabudu wenye uwezo. Fimbo ya mbali haiui nyoka, kwa hiyo unaweza kufanya lolote, naye hatakuwa na cha kufanya zaidi ya kumuachia machozi na sononeko.
Kuna watu hawajiulizi hili; huyo anayekuja kwako akitumia fedha kukuteka kwenye himaya yake, ameshatumia jeuri hiyo kwa wangapi? Endapo utaujua ukweli, utakuja kufahamu kwamba ni wengi aliwanasa kwa sababu alitanguliza fedha.
Weka akilini kwamba haji kwako kwa sababu anakupenda ila anayo jeuri kuwa hutapindua kutokana na fedha alizonazo. Sasa basi, unapomkubalia unamfanya aongeze kiburi. Kesho atatupa ndoano kwa mwingine na huo ndiyo utakuwa mwendo.
Atakutamani kwa sababu ya muonekano wako, kwa hiyo kutokana na kiburi cha fedha alichonacho, kesho akimuona mwingine atakayemtamanisha, atatumia fedha zake kumnasa. Hii ina maana kuwa mkondo wako, watapita wengi. Mwisho kabisa, utabaini kwamba uliingia katika msafara wa kenge.
Atapita kwa wenye tamaa za fedha, nawe utakuja kuingia humohumo. Hii ndiyo sababu ya kusema utajikuta umeunga msafara wa kenge. Wewe utasema unajiheshimu lakini huyo uliyeangukia kwake, hachagui.
Popote kambi, baadaye unapata jawabu kwamba umechangia mwanaume na machangudoa wengi wa mjini.
Tatizo siyo mvuto wako, wapo machangudoa wengi mjini na wanavutia kwelikweli. Kama kavutiwa na wewe na katumia ngawira kukunasa, inashindikana vipi kuvutiwa na machangudoa wengine, nao akatumia fedha kuwanasa? Tena wao si gharama, kwa maana ndiyo kazi yao.
Vilevile kwa mwanaume, atampuuza mtu anayempenda na kumvaa mwingine anayemuona anavutia zaidi. Wengi wamefanya hivyo bila kujua kwamba hao wanaovutia barabarani, asilimia kubwa ni magubegube. Unahitaji mwandani wa maisha yako, tuliza akili.
Sikukatazi kutupa ndoano, ila jaribu kufikiria mara mbili. Uliyenaye hakutoshelezi? Kumuacha mpenzi wa kweli na kujishughulisha na wengine ni sawa na mfano wa mtu aliyepoteza almasi, wakati alipokuwa ‘bize’ akitafuta mawe. Usilie kama wenzako, tuliza akili leo.
Kuna watu wanateseka leo. Wanadai wana mkosi. Eti, mapenzi yanawachapa bakora kwamba hawana bahati nayo. Kama na wewe upo kwenye kundi hili, fumba macho halafu ufikirie ulipotoka. Je, hukumuacha aliyekupenda kwa dhati? Hukuchezea moyo wa yule aliyekuwa anakujali?
Kama jibu ni ndiyo, basi hutakiwi kulia. Mapenzi yalivyo, kupata mwenye moyo mkunjufu katika kupenda ni bahati nasibu. Hivyo basi, kama ulimchezea, ni zamu yako kuteseka kwa maana uliyachezea mapenzi. Ulimpiga teke anayekupenda, sasa unahangaika na wasiokupenda. Wanakuinjoi tu.

Raha za mwenzi wako zipo kwenye himaya yako wewe







 
Wawili wapendanao wakiwa katika huba zito.
Na Kambi Mbwana
MAPENZI ni jambo ambalo linaleta hisia mbili tofauti. Mosi; mapenzi yanaweza kukufanya uishi kwa raha kama mfalme. Pili, mapenzi hayo yakibadilika hukufanya uwe kama chizi.

Jambo hilo zuri linalofananishwa na sukari kwa yaliyowakalia vizuri, hubadilika na kuwafanya baadhi yao waone ugumu wa kuendelea kuishi, maana wanaowapenda wanawasumbua kwa kiasi kikubwa.

Ni kutokana na hilo, jamii inashauriwa kuwa makini katika suala hilo. Wasijaribu kukurupuka na kuchukua uamuzi wenye mashaka kwa namna moja ama nyingine, maana vinginevyo watatamani kujinyonga.

Hata hivyo, pamoja na yote hayo, lakini inajulikana wazi wazi kuwa dawa kubwa katika uhusiano wa kimapenzi ni kumfikisha mwenzako, kumuweka katika kilele cha ubora katika ulimwengu wa mapenzi.

Katu usiangalie umbo lako, sura yako katika kujigamba kwamba unaweza kupendwa na yoyote, wakati ni mzigo kitandani. Kama huna ujuzi katika suala la mapenzi, ondoa kupendwa, kuhitajiwa au kugandwa na yoyote.

Zaidi ya hapo, wachache wao watakupitia na kuchukua hamsini zao, maana huna ujanja wa kumuweka mwenzako katika furaha. Hivyo basi, ili jamii iwe kwenye ramani nzuri na furaha ya mapenzi, lazima tuwajulie watu wetu.

Tufahamu namna ya kuwachanganya kisaikolojia, bila kuangalia uzuri wetu, fedha zetu, maana hizo haziwezi kufanya penzi liwe na amani.

Wapo ambao wanaishi na wanaume wenye nazo kupita kiasi, lakini bado wake zao, wachumba zao au wapenzi wao wanajiingiza katika uhusiano na watu wa kawaida, wakiwamo wafanyakazi wa ndani.

Hata hivyo haitoshi, wapo pia wakina mama wenye nazo lakini wanachanganywa na wasichana wa kawaida, wenye sura za kawaida au hadhi za kawaida. Wenye mali zao wanalia na kusaga meno.

Wanasema“Hivi kwani mume wangu unatembea na yule mfanyakazi wa ndani wakati mimi nipo” Au sielewi unachofuata kwa yule kijana mchunga mbuzi wakati mimi nipo, tena mwenye fedha za kutosha tu”

Kama wewe ni miongoni mwa watu wenye mtazamo huo umeliwa. Fedha sio kila kitu katika mapenzi. Fedha zako usipoangalia zinaweza kuwanufaisha wapita njia, wajuzi wa mambo kwenye mambo fulani muhimu.
Huo ndio ukweli wa mambo. Mjuzi huyo hatafutwi ili mradi mtu ana mtu wa nje, ila umuhimu wake unakuja anapokuwa kwenye ulingo. Hayo lazima mimi na wewe tuyajuwe kwa ajili ya mapenzi yetu.

Unapokuwa na mpenzi wako, mume au mke wako lazima ujuwe yupo na wewe kwa ajili ya kujenga maisha ya wawili. Ili mwenzako afurahie uwepo wako, hakikisha kuwa walau unatumia muda wako hata kama kidogo kumridisha kimapenzi.

Kwa wale ambao kwa miaka mingi wameishi na wapenzi wao bila kutumia ujuzi wao, waanze leo. Na wale wanaoingia kwenye uhusiano leo, pia wawaangalie watu wao, namna gani walivyo na wanastahili aina gani ya mapenzi.

Ninaposema mapenzi, sio yale ya kukaa pamoja, kutembea pamoja au kumpigia simu kila baada ya dakika kumi. Mapenzi, tendo la ndoa lenye ujazo mkubwa linalostawisha uhusiano wa wawili wapendanao.

Hivyo basi tuwe makini katika kazi hiyo. Tukitaka kuwapa raha kweli wenzetu lazima tuache kazi na kufanya kazi. Tendo la ndoa sio mchezo mdogo. Sio kama kuwasha njiti ya kibiriti mahala palipotulia.

Inahitaji kusumbua akili na kusumbua pia mwili wako. Sina maana kama nataka muda wote muwe kwenye tendo la ndoa, ila mnapotaka kufunja amri hiyo ya sita, basi mfikishe mwenzako kileleni.

Usimchezee chezee tu ukamuacha. Nimeamua kuandika mada haya maana nimepata malalamiko mengi kutoka kwa wanawake. Baadhi ya wasomaji wangu, wamenipasha kwamba waume zao ni watu wa kwenda raundi moja halafu wanaangalia ukutani.

Kwa bahati mbaya, watu hao wanapolala uzungu wa nne, wanakuwa wanawanyanyasa wenzao, kama unavyojua tena gari linapowaka. Hali hiyo inakera kiasi cha kutamani wapiti njia.
Haya nayasema kwa uchungu, maana usaliti mwingi huibuka kama wawili wapendanao hawaridhishani. Kama unaona huna ujuzi wa kumuweka katika kilele mwenzako, tafuta msaada kwa watu.